
Maandamano makubwa yanapangwa
kufanywa sehemu mbalimbali Brazil, ambako wabunge wanatarajiwa kupiga
kura leo, ikiwa wanataka Rais Dilma Rousseff ashtakiwe au la, kwa sababu
ya kubadilisha bajeti. Wanaompinga lazima wapate thuluthi mbili ya kura
zote , kuweza kumshtaki rasmi kiongozi huyo katika baraza la Seneti.

Waandishi wa habari wanasema, kizuizi cha urefu wa mita mbili, kilichowekwa baina ya waandamanaji hao, mahasimu ni ishara ya mgawanyiko mkubwa nchini, baina ya wafuasi na wapinzani wa Rais Rousseff.

Anawashutumu wanasiasa wanaotaka kuitoa madarakani serikali iliyochaguliwa.
No comments:
Post a Comment