Total Pageviews

Sunday, April 17, 2016

Kenyatta akosoa kauli ya Odinga



                              Rais wa Ufaransa, François Hollandeakimpokea  Ikulu ya Elyséemwenzake wa Kenya, Uhuru Kenyatta, Jumatau Aprili 4, 2016.
Rais wa Ufaransa, François Hollandeakimpokea Ikulu ya Elyséemwenzake wa Kenya, Uhuru Kenyatta, Jumatau Aprili 4, 2016.

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amekosoa kauli ya kinara wa muungano wa upinzani na Waziri Mkuu wa zamani Raila Odinga, kuwa hatua ya Mahakama ya Kimataifa ya ICC kutupilia mbali kesi dhidi yake Kenyatta na naibu wake William Ruto si sahihi.

Akizungumza akiwa nchini Ufaransa, Odinga alisema hatua hiyo ya ICC ilkuwa ni pigo kwa jitihada za kupigania haki hasa baada ya uchaguzi Mkuu wa mwaka 2007.

Rais Kenyatta anasema, matamshi ya Odinga yanalenga kuwaharibia jina.
Kauli ya Kenyatta imeungwa mkono na Naibu wake Ruto ambaye amesema wale waliomsingizia wameshindwa.

Aden Duale naye ni kiongozi wa walio wengi bungeni, amepomgeza msimamo wa viongozi hao wawili.
Mahakama ya ICC ilisitisha kesi dhidi ya viongozi wa Kenya kwa ukosefu wa ushahidi.

No comments:

Post a Comment