Rais wa Urusi Vladimir Putin amekanusha madai ya kutakatisha mabilioni ya pesa.
Rais
Putin anasema kuwa hakuna ukweli wowowte katika madai hayo na kuwa hizo
ni njama za mahasidi wake za kutaka kuiyumbisha serikali yake.Putin alikuwa akizungumzia kwa mara ya kwanza kasha la nyaraka za siri za kampuni moja ya kisheria ya Panama, Mossack Fonseca iliyomtaja mshirika wake mmoja wa karibu kuwa alitakatisha mabilioni ya dola .
Stakabadhi hizo za siri za Mossack Fonseca zilizopatikana na gazeti moja la Ujerumani zilionyesha kuwa viongozi zaidi ya 72 wakuu wa nchi wa zamani na wale waliopo madarakani wanahusika na kampuni hiyo ya kisiri iliyowasaidia
Aidha kampuni hiyo ya Mossack Fonseca imewasaidia watu duniani kote kufungua kampuni hewa kwenye visiwa ambavyo havitozi kodi.
Hati hizo zinaonyesha kuwa dola bilioni kadhaa zilitakatishwa na benki moja ya Urusi kwa kumuhusisha mtu mwenye uhusiano wa karibu na rais Urusi Vladimir Putin.

No comments:
Post a Comment